slider gif

slider gif

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

Tuesday, August 15, 2017

ZIARA YA MANAIBU WAZIRI WATATU UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA WA JULIUS NYERERE NA MAMLAKA YA BANDARI TANZANIA

Naibu Waziri wa Maliasili, Mhandisi Ramo Makani (wa tatu kulia), Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni (wa nne kulia) na Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Edwin Ngonyani (wa tano kulia) wakimsikiliza Mkuu wa Kitengo cha Uzingatiaji wa Viwango wa Mamlaka ya Viwanja wa Ndege, Paul Rwegosha wakati wa ziara yao ya pamoja ya kukagua maeneo ya kuingilia wageni wa kimataifa hususan watalii katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Dar es Salaam kwa ajii ya kubaini changamoto na kuziboresha ikiwa ni pamoja na kuziba mianya ya mapato ya Serikali yanayotokana na watalii wanaoingia nchini.
Naibu Waziri wa Maliasili, Mhandisi Ramo Makani (wa pili kulia) akizungumza katika kituo cha "terminal III" cha Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es Salaam kinachoendelea kujengwa wakati wa ziara ya pamoja na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamadi Masauni (wa tatu kulia) na Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Edwin Ngonyani (kulia) kwa ajili ya kukagua maeneo ya kuingilia wageni wa kimataifa hususan watalii katika uwanja huo kwa ajii ya kubaini changamoto na kuziboresha ikiwa ni pamoja na kuziba mianya ya mapato ya Serikali yanayotokana na watalii wanaoingia nchini.
 Mkuu wa Kitengo cha Uzingatiaji Viwango wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini, Paul Rwegasha, akifafanua jambo wakati wa ziara iliyojumuisha  Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Edwin Ngonyani(kushoto), Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani (wapili kushoto)  na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(kulia).Lengo la ziara hiyo ni kukagua masuala mbalimbali ikiwemo Ulinzi, Usalama, Miundombinu,Utolewaji wa visa, uingiaji na utunzaji kumbukumbu za Watalii wanaoingia nchini.
Meneja Huduma za Abiria wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere, Damas Temba, akielezea jinsi huduma ya kukagua mizigo inavyofanyika katika sehemu ya mizigo wakati wa ziara ya Manaibu Waziri, Mhandisi Hamad Masauni (Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi), Mhandisi Ramo Makani(Wizara ya Maliasili na Utalii) na Mhandisi Edwin Ngonyani(Wizara ya UIjenzi, Uchukuzi na Mawasiliano), ikiwa na lengo kukagua masuala mbalimbali ikiwemo Ulinzi, Usalama, Miundombinu, Utolewaji wa visa, uingiaji na utunzaji kumbukumbu za Watalii wanaoingia nchini.
Meneja Mradi Ujenzi wa Uwanja Mpya wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Ray Blumrick, akizungumza na Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni baada ya kumaliza kutembelea ujenzi huo.Lengo la ziara hiyo ni kukagua kukagua masuala mbalimbali ikiwemo Ulinzi, Usalama, Miundombinu, Utolewaji wa visa, uingiaji na utunzaji kumbukumbu za Watalii wanaoingia nchini.
Naibu Mkurugenzi Mamlaka ya Bandari Tanzania, Lazaro Twange (katikati), akiwaonyesha ramani ya bandari ya Dar es Salaam, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani(kulia) na Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni wakati wa ziara ya viongozi hao lengo ikiwa ni kukagua masuala mbalimbali ikiwemo Ulinzi, Usalama, Miundombinu, Utolewaji wa visa, uingiaji na utunzaji kumbukumbu za Watalii wanaoingia nchini.
Naibu Mkurugenzi Mamlaka ya Bandari Tanzania, Lazaro Twange,  akifafanua jambo kwa  Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani(wapili kulia) na Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni (kulia), wakati wa ziara ya viongozi hao, lengo ikiwa ni kukagua masuala mbalimbali ikiwemo Ulinzi, Usalama, Miundombinu, Utolewaji wa visa, uingiaji na utunzaji kumbukumbu za Watalii wanaoingia nchini.Kushoto ni Mkuu wa Kikosi cha Polisi Bandarini,Matanga Mbushi.

No comments:

Post a Comment